Sabtu, 10 Desember 2011

EXCLUSIVE INTERVIEW WITH DJ CHOKA (AUTHENTIC & APPROVED)



DJ Choka


"Maisha ni kuendelea hadi zamu yangu ya kushinda ifike. Sikatishwi tamaa na kushindwa ndipo nitaona kuwa ugumu nikipindi cha mapito kuelekea mafanikio"




Kachumbari C: Jina lako la ukweli ni lipi?

DJ Choka: Hugoline Martin Mtambachuo


Kachumbari C: Nini kilichokufanya uwe DJ?

DJ Choka: Kilichonifanya niwe DJ nikutokana na kuona madj wa nje wakiwa wanafanya kazi zao na
                  wasanii so na me nikapenda kuwa dj wa wasanii na kuwa tofauti na dj wa harusi au dj wa
                  radio


Kachumbari C: Ni vizingiti gani vikuu unavyokumbwa navyo kwenye u-DJ?

DJ Choka: Viko vingi unaweza kwenda sehemu na msanii ukakuta waandaaji wameandaa mashine
                  mbaya mbovu inabagua cd halafu kinachofuata ni kuaribu show ya msanii uliyekwenda nae
                  halafu mashabiki wanakuwa hawakuelewi wanajua ni mimi nimefanya makusudi.


Kachumbari C: Unadhani nini kifanyike ili kukuza na kuifaidisha sanaa ya muziki Tanzania?

DJ Choka: Kinachotakiwa kifanyike ni sisi wananchi kupenda sanaa ya nyumbani na kununua kazi za
                  wasanii wanaposikia album ya msanii imetoka na kuacha ulimbukeni wa kuchoma nyimbo
                  kwenye vibanda


Kachumbari C: Ni wasanii gani wa Bongo unaowakubali?

DJ Choka? Wako wengi sana ila kuna wale ambao mara kwa mara nakuwa nao na nafanya nao kazi
                   kama wakinichukua, kuna kaka yangu Prof Jay, AY, Mwana FA, Joh Makini, Jay Moe,
                   Roma, Fid Q, Mo Racka, Quick Racka, JCB, Nako 2 Nako nk

DJ Choka akiwa na kaka yake Prof. Jay

Mwana FA


AY akiwa na Romeo

Kachumbari C: Ni wasanii gani wa nchi za nje unaowakubali?

DJ Choka: Busta, Rick Ross, Ludacris, Eminem, Dj Khalid, Lil Wayne, Nick Minaj, 50 Cent, nk


Busta Rhymes

Nicki Minaj 


Kachumbari C: Unadhani msanii gani chipukizi atakuja kung'aa sana hapo mbeleni?

DJ Choka: Mimi nadhani Dogo Janja na Dogo Asley kutoka TMK Wanaume Family

Dogo Asley

Dogo Janja


Kachumbari C: Kwa mtazamo wako,ili msanii aweze kung'aa katika sanaa ya muziki Bongo,awe na 
                         vitu gani?

DJ Choka: Awe msafi tu..avae vitu vizuri kulingana na kazi yake anayoifanya, na kila siku atunge 
                  nyimbo nzuri zitakazokubalika na jamii


Kachumbari C: Wasanii gani wa Bongo Movies unaowakubali?

DJ Choka: Kanumba, JB, Ray, Yusuph Mlela, Mdogo wangu Lulu, Jack Wolper, Aunt Ezekiel

Kanumba


Jacqueline Wolper


Ray akiwa na Mh.Jakaya M. Kikwete

Kachumbari C: Mashabiki wako wategemee nini kutoka kwako mwaka 2012?

DJ Choka: Wategemee vitu vizuri tu, mimi sipendi kuahidi vitu halafu nisitimize so tunaomba pumzi tu 
                  na nguvu ili malengo yatimie. ONE



Tidak ada komentar:

Posting Komentar